Mungu Wa Mapendo (God of Love) Lyrics by Rose Muhando

1 Comment



(Sung in Swahili)

Nini kitanitenganisha (na upendo wa Mungu Baba)
(What can separate me, from the Love of God the Father)
Ikiwa ni dhiki au njaa (Havitananitenga naye Baba)
(Neither hardship nor famine, shall separate me from the Father )
Mauti, upanga, na dhihaka (Havitananitenga naye Baba)
(Death, war and danger, will not separate me from the Father)
(Repeat)

Chorus:
Sina hofu sibabaiki (I’m not afraid, not worried)
Kwake yeye nime/nitashinda (I have/shall won/win)
Milele yote nime/nitashinda (Forever I have/will win/won)
Tena zaidi ya kushinda (Even more than win)
Kwake yeye aliyenipenda (In Him who loved me)
(Repeat)

Kwenye zamu yangu nitasimama (When my turn comes I shall stand)
Kwa miguu yangu nitasimama (On my feet I shall stand)
Nione Bwana atakavyonijibu mimi (To see what the Lord shall say to me)
Kwa habari ya kulalamika kwangu (Regarding my persecutions)
Bwana aliniambia neno hili (As the Lord had promised me)
“Usiogope maneno yao (“Do not fear their words,)
Usitetemeke mbele yao, (Do not tremble before them)
usifadhaike mbele yao (Do not despair before them )
Maana imeandikwa, kwa ajili yako ninauawa (As it is written, I was killed for your sake)
kama kondoo wa kuchinjwa, kifo nimehesabiwa (Like a lamb to slaughter, in your death you were counted)
Kifo nimehesabiwa, mimi sibabaiki (In my death I have been counted, I am not worried)

Bridge:
Shetani usinisumbue (Shetani usinisumbue) (Satan, do not bother me)
Wala usinibababishe (Wala usinibababishe) (Do not worry me)
Funga kinywa ukatoweke (Funga kinywa ukatoweke) (Be quiet and begone)
Nyamaza kimya ukapotee (Kwa jina la Yesu ukatoweke) (Be silent and be gone in the name of Jesus)
Nyamaza kimya ukapotee (Nyamaza kimya ukapotee) (Be quiet and begone)

(Chorus)

Milele neno la Mungu limehakikishwa (Forever the word of God has been established)
Tena ni ngome kwa wamwaminio (It is a fortresses to the believers)
Tena ni ngao kwa wamwitao Baba (Also a shield for those who call him Father)
Kabla ijawa misingi ya dunia, (Before the foundation of the world)
Yeye huyu alikuweko (He was here)
(?), muumba wa utukufu ([?], Creator of glory)
Na utakaso wa dhambi, (?) (And the cleansor of sin, (?))
Nami kwake ni wa mwana x2, ni wa mwana (I belong to the son)

(Bridge) + (Chorus)

Asifiwe Mungu wa mapendo (God of love be praised)
Asifiwe Mungu wa huruma (God of mercy be praised)
Asifiwe Mungu wa amani (God of peace be praised)
Asifiwe Mungu wa mapendo (God of love be praised)

Asifiwe Mungu wa mapendo (God of love be praised)
Ametenda maajabu, (He has done amazing things)
dunia ishangilie (Let the world rejoice)
Visiwa(?) vitoe nyimbo, (All islands  give praise)
Asifiwe Mungu wa mapendo (God of love be praised)

Mungua chukua heshima yako (Gpd receive your honor)
Mungu chukua utukufu wako (God receive your praise)

Asifiwe Mungu wa mapendo (God of love be praised)
Ametenda maajabu, (He has done amazing things)
dunia ishangilie (Let the world rejoice)
Visiwa(?) vitoe nyimbo, (All islands  give praise)
Asifiwe Mungu wa mapendo (God of love be praised)
(Repeat)

Utamu wa Yesu (The Sweetness of Jesus) Lyrics by Rose Muhando

7 Comments



(Sung in Swahili)

Lile lile…

Acheni muone utamu wa Yesu we (Let me show the sweetness of Jesus)
Mama we onjeni utamu wa Yesu we (Come and taste the sweetness of Jesus)
Mwenzenu nimeonja utamu wa Yesu we (I have tasted the sweetness of Jesus)
Usione nina raha nimeonja utamu wa Yesu we
(See my joy, I have tasted the sweetness of Jesus)
Si kama nimechanganyikiwa bali ni utamu wa Yesu we
(I’m not crazy, it is the sweetness of Jesus)
Jamani sijarukwa na akili bali utamu wa Yesu we
(I am not mad, but it’s the sweetness of Jesus)
Utamu we, nimeonja utamu we x2 (The sweetness, I have tasted the sweetness)

Chorus:
Utamu we, nimeonja utamu we he x2 (The sweetness, I have tasted the sweetness)
Utamu wa Yesu we, Utamu wa Yesu we x2 (The sweetness of Jesus)
Utamu we, utamu x3 (The sweetness)
Utamu wa Yesu we, he (The sweetness of Jesus)
Mwemere, mwemere x4 (?)

Viko vingi vitamu lakini mwisho wake mauti (A lot of pleasures lead to death)
Viko vingi vitamu lakini mwisho wake kilio (A lot of pleasures lead to tears)
Vingine ni vitamu lakini mwisho wake kilio (Others are pleasurable but lead to tears)
Ni vitamu lakini mwisho vichungu kama shubiri (Are pleasurable but end in bitterness)
Ni vitamu lakini mwisho vinawasha kama upupu (Are pleasurable but end with disease)
Ni vitamu lakini mwisho vinapalia we (The are pleasurable, but only fleetingly)
Acheni niuseme utamu wa Yesu we (Let me testify on the sweetness of Jesus)
Wacheni nisifu utamu wa Yesu we (Let me praise the sweetness of Jesus)
Umetutenga mbali na dhambi, utamu wa Yesu we
(It has separated us from sin, the sweetness of Jesus)
Haufanani na utamu wa asali, utamu wa Yesu we
(It cannot be compared to honey, the sweetness of Jesus)
Thamani yake imeshinda almasi, utamu wa Yesu we
(It’s value exceeds that of a diamond, the sweetness of Jesus)
Ni mali ghafi isiopatika kwa mapesa jamani he
(It is a rare jewel that cannot be bought)
Bali kwa njia ya msalaba tumepewa utamu wa Yesu we
(But by the way of the cross, we have been given the sweetness of Jesus)
Mbinguni tunakwenda bure, uzima tunapata bure
(To heaven we go for free, we are given eternal life for free)
Wokovu tumepata bure, amani tunapata bure
(We have been given free salvation, peace we find for free)
Utamu we, nimeonja utamu we x2 (The sweetness, I have tasted the sweetness)

(Chorus)

Umetutenga mbali na dhambi, utamu wa Yesu we
(It has separated us from sin, the sweetness of Jesus)
Usione tuna raha, tumeonja utamu wa Yesu we
(We are joyful as we have tasted the sweetness of Jesus)
Usione tunacheka, tumeonja utamu wa Yesu we
(We laugh as we have tasted the sweetness of Jesus)
Umetutenga mbali na dhambi, utamu wa Yesu we
(It has separated us from sin, the sweetness of Jesus)
Umetusogeza karibu na Mungu, utamu wa Yesu we
(brought us close to God, the sweetness of Jesus)
Dhambi zetu zimewekwa mbali na Mungu, utamu wa Yesu we
(Our sins are forgiven, the sweetness of Jesus)
Walio chini wameinuliwa, utamu wa Yesu we
(The last are first, the sweetness of Jesus)
Badala ya kilio ni kicheko, utamu wa Yesu we
(Joy instead of tears, the sweetness of Jesus)
Badala ya aibu utukufu, utamu wa Yesu we
(Praise instead of shame, the sweetness of Jesus)
Mito ya baraka inatiririka, utamu wa Yesu we x2
(The springs of blessings flow, the sweetness of Jesus)
Utamu we, nimeonja utamu we (The sweetness, I have tasted the sweetness)

(Chorus)

Mkitaka magari mazuri, onjeni utamu wa Yesu we
(You want to be blessed with cars, taste first the sweetness of Jesus)
Mkitaka majumba mazuri, onjeni utamu wa Yesu we
(You want to be blessed with houses, taste first the sweetness of Jesus)
Mkitaka kubarikiwa, onjeni utamu wa Yesu we
(You want to be blessed, taste first the sweetness of Jesus)
Mkitaka kuinuliwa, onjeni utamu wa Yesu we
(You want to be lifted, taste first the sweetness of Jesus)
Utamu we, nimeonja utamu we (The sweetness, I have tasted the sweetness)

(Chorus)

Sing’oki ng’o, kwa Yesu sing’oki ng’o x4 (No, I will not leave Jesus)
Utamu we, utamu x3 (The sweetness)
Utamu wa Yesu we (The sweetness of Jesus)

Mungu Wangu Nitakushukuru (My God I Will Thank You) by Rose Muhando

8 Comments



(Sung in Swahili)

E mungu wangu mimi ninatukushukuru (O my God I will thank you)
Mbele ya mataifa mimi nitaimba (Before the nations I will sing)
Dunia nzima nayo itambue hilo (All the world to know that)
Kwamba jina la yesu pekee ndilo (The name of Jesus alone)
Ulimwengu mzima uokolewe kwalo (that will save the world)

Asubuhi na mapema, mimi nitaimba (Early in the morning, I will sing)
Kabla ya kinywa kunena, kwako nitaimba (Before my mouth speaks, I will sing)
Tufani ijapozidi wo, kwako nitaimba (Though troubles increase, to you I will sing)
Nijapoteswa kabisa, kwako nitaimba (Though I am persecuted, to you I will sing)
Nijapodharauliwa, kwako nitaimba (Though I am hated, to you I will sing)

Chorus:

Swiyi… Sikia e kinanda (Swiyi …. listen you guitar)
Swiyi… Amka we kinubi (Swiyi… rise you flute)
Swiyi… Sikia e kinanda (Swiyi… you listen you guitar)
Inuka e zumari, inuka kwa sauti (Rise you flute, rise aloud) (x2)
Woo na utukuzwe Mungu, Woo na utukuzwe Mungu, (God be praised)
Yee Jehova adonai, Yee Jehova adonai, (Jehova Adonai)
El gibo shalom mungu unaitika (El Gibo Shalom, God you answer)
El gibo shalom mungu unaitika (El Gibo Shalom, God you answer)

Uniondolee majivuno, komesha kiburi (remove my boast, stop my pride)
Utawale akili zangu, Bwana niongoze (rule my thoughts, Lord lead me)
Unifundishe roho yangu habari za mbingu (teach my spirit, the things of heaven)
Sikizeni eh kizazi changu, Mungu anaishi (listen my generation, God lives)
Uniondolee majivuno, komesha kiburi (remove my boast, stop my pride)
Utawale akili zangu, Bwana niongoze (rule my thoughts, Lord lead me)
Unifundishe roho yangu habari za mbingu (teach my spirit, the things of heaven)
Sikizeni eh kizazi changu, Mungu anaishi (listen my generation, God lives)

(Chorus)

NIpe moyo ya nyama, ulopondeka (Give me heart of flesh, that is teachable)
Moyo uliotulia, na unyeyekevu (a peaceful and humble heart)
Mimi si kitu kwako, ni mdhuru? tu (I am nothing but dust to you)
Mimi ni kama nani, uniinue (who am I that you should raise me?)
Unifinyange bwana, kama upendavyo (Mould me Lord, the way you like)
Unifundishe Bwana kama upendavyo (Teach me Lord, the way you like)

(Chorus)

NIkikuita mungu, unaitika (When I call you God, you answer)
Rohi eloie heika (?), noishikimu (…Hebrew (?))
Jira el shadai, Jehova oseenu(…Hebrew (?))
El elyo shammah, Mungu unaitika (…, God you answer)
Jehova shabbah, Mungu utanijibu (Jehova Shabbah, God you will answer me)
El gibo shalom, Mungu unaitika (El gibo Shalom, God you answer)
El gibo shalom, Mungu unaitika (El gibo Shalom, God you answer)
El gibo shalom, Mungu unaitika (El gibo Shalom, God you answer)

(Chorus)

Nipishe Nipite (Let Me Pass) by Rose Muhando

2 Comments



(Sung in Swahili)

Nakuuliza shetani umepata wapi mamlaka
(I ask you devil, where did you get the permission)
Ya kukamata akili za watu ah! (To mess with people’s minds)
Wewe umeleta balaa umeingia makanisani
(You’ve brought trouble, you have gotten into churches)
Umekamata wababa wanabaka watoto wao
(You have made fathers to rape their children)
Umekamata vijana umewatwika ulevi
(You have caught young men, and saddled them with alcoholism)
Bila kusahau kina mama, vikao vya masengenyo
(Not forgetting mothers, and their gossip)
Sasa nimechoka na mambo yako (I’m tired of your work)
Ewe shetani, nipishe nipite (You Satan, let me pass)

Chorus:
Wewe ulimwasi Mungu, nipishe nipite (You who defied God, let me pass)
Uliwadanganya adamu na Eva, songea nipite
(You deceived Adam and Eve, move and let me pass)
Dunia nzima imeharibika, kwa ujanja wako
(The world is destroyed, for your cunning)
WEwe ulimwasi mungu, nipishe nipite (You who defied God, let me pass)
Uliwadanganya Adamu na Eva, songea nipite
(You deceived Adam and Eve, move and let me pass)
Dunia nzima imeharibika, kwa ujanja wako
(The world is destroyed, for your cunning)
wewe shetani unaambiwa, mwenyeji wa kuzimu (
You Satan you’ve been ordered, the host of hell)
Sasa nipishe nipite (Now let me pass)

Hebu nipishe nipite, ninachelewa njiani (Let me pass, I’m getting late)
Yesu yu karibu kurudi, kulichukua kanisa
(Jesus is almost returning to take his church)
Kanda unayo nionyesha yote yamepitwa na wakati
(Whatever you show me has been passed by time)
Huna ujanja (You can’t fool me)
Kumbuka miaka elfu mbili iliyopita zamani (Remember 2000 years ago)
Yesu aliposhuka kuzimu, akakunyanganya funguo
(When Jesus descended to hell, and took the keys)
Funguo za mamlaka (The keys of authority)
Nasema nimechoshwa na mambo yako (I say I am tired of you)
Wewe shetani nipishe nipite (You devil, let me pass)

(Chorus)

Nakuamuru shetani wewe, nipishe nipite (I order you Satan, let me pass)
Wewe umekuwa ni kikwazo kwangu, Kufika mbinguni
(You have been my barrier to heaven)
Muda wako umeshakwisha, songea nipite (Your time is up, let me pass)
Sasa haleluya naenda mbinguni, hakuna mashaka
(Now Hallelujah I’m going to heaven, no worries) (Repeat)

Wewe ulishaaniwa, laana milele (You have been cursed forever)
Ulinyanganywa mamlaka na Yesu, Huna ujanja ee
(You’re authority was taken by Jesus, you have no more cunning)
Simba wa yuda aliponguruma, mafuriko kuzimu
(When the Lion of Judah roars, there is flood in hell)
Sasa haleluya twaenda mbinguni, hatuna mashaka
(Now hallelujah we are going to heaven, no worries) (Repeat)

(Chorus)

Heshima (Respect) Lyrics by Annastazia Mukabwa And Rose Muhando

3 Comments



(Sung in Swahili)

Refrain:
Wanaokudharau siku moja watakusalimia kwa heshima
(Those who despise you, one day will greet you with respect)
(repeat)

Mateso yako ni ya muda tu, Mungu akuandalia ushuhuda
(Your troubles are only for a time, God is preparing a testimony for you)
Daudi Alikuwa mchunga kondoo, Mungu akamwinua kuwa mfalme
(David was a shepherd, God lifted him to be a king)
Leo unaitwa ombaomba, kesho utaitwa mbarikiwa
(Today you are called a beggar, tomorrow you will be called blessed)
Licha unatembea kwa miguu, kesho utaendesha gari
(Inspite of walking, tomorrow you will drive a car)

Chorus:
Nasema watakusalimia, kwa heshima (I say they will greet you, with respect)
Watakusalimia, kwa heshima (They’ll greet you with respect)
Wakati wako wako wa kuinuliwa, ukifika (When your time to be lifted, has come)
Watakusalimia, kwa heshima (They will greet you, with respect)
Wakati wako wa kubarikiwa, ukifika (When your time to be blessed, arrives)
Watakusalimia, kwa heshima (They’ll greet you with respect)
Wakati wako wa kukumbukwa, ukifika (When your time to be remembered arrives)
Watakusalimia, kwa heshima (They’ll greet you with respect)

Wanaosema hautaolewa, watashuhudia ndoa yako
(Those who say you will not be married, will witness your wedding)
Pale utakapovalishwa pete, watashikwa na kigugumizi
(When you are given a ring, they will be speechless)
Wanaosema wewe ni tasa, watakuona ukinyonyesha
(Those who say you are barren, will see you breastfeeding)
Na Mungu alimkumbuka Sara, hata wewe utakumbukwa
(God remembered Sarah, he will remember you as well)

(Chorus)

Wakuu wa Mungu wetu ni Ebeneza, hata sasa yupo
(Our great God is Ebenezer, even now he is here)
Msaada wetu wa karibu, mwite ataitika
(Our close help, call him and He’ll answer)

Jifunze kuwa na subira, utafanikiwa
(Teach yourself to be patient, and you will succeed)
Sana siku sio gani mama, atakuinua
(Not for much longer mother, he’ll lift you up)
Ona leo wanakuita kikaragosi, kesho watakuita bosi
(Look today they call you useless, tomorrow they’ll call you boss)
Aliyekunyima kadi za harusi, kesho wataomba shela yako
(Those who denied you an invitation, tomorrow will beg for crumbs)
Ona leo wanakupiga kibuti, kesho watakupigia saluti
(Today they kick you out, tomorrow they’ll salute you)

Watakusalimia, kwa heshima (They’ll greet you with respect)
Watakupigia magoti, ukifika (They’ll kneel before you, when you arrive)
Watakusalimia, kwa heshima (They’ll greet you with respect)
Walikuona ukilala jalani, ukifika (They saw you sleeping on rubbish, when you arrive)
Kesho watakupata ofisini, kwa heshima (Tomorrow they’ll find you in your office with respect)
Watakusalimia, ukifika (They’ll greet you when you arrive)
Watakusalimia, kwa heshima (They’ll greet you with respect)
Watakupigia saluti, watakusalimia kwa heshima.
(They’ll salute you, they’ll greet you with respect)

Older Entries Newer Entries