Chorus:

Mungu amekusudia kukubariki
Mungu amekusudia kukubariki

Verse 1:

Je unaweza kungojea kidogo
Kwani bwana yesu amekusudia kukubariki
Mateso unayopitia siku ya leo
Hayalinganishwi na utukufu utakaopata

(chorus)

Verse 2:

Je unajua kucheleweshwa si kunyimwa
tena kungojea huzaa kuvumilia
Kuvumilia huzaa kukomaa
Heri kukomaa kuliko kuwa mtoto

(Chorus)

Verse 3:

Kumbuka Hana alimgojea Bwana
Akabarikiwa na nabii Samweli
Huyo Mungu aliyemkumbuka
Siku ya leo atakukumbuka

(Chorus)

Verse 3:

Iburahimu allimgojea Mungu
Miaka mia moja Mungu hakumsahau
Anyeshaye mvua jangwani
Atakuinua watu washangae

(Chorus)

Verse 4:

Nakuhakikishia ewe rafiki yangu
Kwamba Mungu wangu ni mwaminifu
Usihangaike mngojee Bwana
Ahadi zake hazivinjiki milele